Tuesday, December 25, 2012

GHARAMA YA KUMFUATA KRISTU



   
                         SIKUKUU YA MT.STEFANO SHAHIDI
                              
                                    26 Desemba 2012

  1. 1. Mate 6: 8-10, 7: 54 -59
Mt 10: 17-22


UTANGULIZI

Jana ilikuwa “Birthday” ya Yesu Kristu. Leo ni Birthday ya Mtakatifu Stefano shahidi. Ni kuzaliwa kwa Mtakatifu Stefano. Lakini ni kuzaliwa kwake mbinguni. Sikukuu ya Mtakatifu Stefano inavumbua mbivu na mbichi katika kumfuata Yesu Kristu. Ili tuzaliwe mbinguni hatuna budi kulipa gharama. Jana Bwana alizaliwa duniani ili Stefano azaliwe mbinguni. Jana aliingia duniani ili Stefano aweze kuingia mbinguni.

GHARAMA YA KUMFUATA KRISTU

MSAMAHA

Stefano aliwasamehe wauaji wake. Alisema, “Bwana, usiwalaumu kwa sababu ya dhambi hii” (Matendo 7:60). Msamaha ni gharama ya kumfuata Yesu Kristu. Watu hujiandaa kusamehe lakini walio wengi hawajiandai kusamehewa. Je kama unasemehewa unapokea msamaha? Bwana Yesu alipokuwa kufani msalabani alisema maneno saba msalabani: Neno la kwanza ni: “Baba, uwasamehe kwa maana hawajui wanalofanya,” (Luka 23: 34). “Kufanya makosa ni jambo la kibinadamu, kusamahe ni jambo la kimungu,” Alisema Alexander Pope (1688-1744) mshairi wa Uingereza. Lakini tujue kuwa kuendelea kutenda makosa bila kuacha ni jambo la kishetani. Yesu alivyowasamehe waliomkosea alifanya jambo la kimungu. Hakutaka kutwika uwezo wake wa kukumbuka mzigo mzito wa mambo yaliyopita. Kama yeye alifanya hivyo kwa nini sisi tunabeba mizigo mizito ya mambo mabaya tuliyotendewa.

William Shakespeare aliandika hivi katika kazi yake iitwayo, “The Tempest,” “Prospero, alipopewa nafasi kuwaadhibu wale waliomwondoa katika nafasi yake kama mfalme, alisema, ‘Tusitwishe mzigo mzito kumbukumbu zetu kwa jambo zito ambalo limepita.” Kununa kwetu hakubadili historia. Kukasirika kwetu hakubadili historia. Kulaani hakubadili historia. Kutukana hakubadili historia. Kusamehe kunabadili historia maana hakuongezi idadi ya watu wabaya lakini kulipiza kisasi kunaongeza idadi ya watu wabaya.

Bwana Yesu ni kioo cha jamii na familia katika kutoa msamaha. Aliwatetea waliomfanyia mabaya kuwa hawakujua. Wanafamilia wajifunze toka kwa Yesu kusameheana. Maneno “nisamehe” yawe kama kiitikio katika familia. Familia ni shule ya kwanza ya kujifunza kusamehe na kupokea msamaha. Wazazi ni walimu wa kwanza wa somo la msamaha. Kama pametokea ugomvi, msamaha ufuate kama asubuhi inavyofuata usiku. Ugomvi huanza kwa kutokubali kosa na kuomba msamaha. Mfano, mtu mmoja alimwambia mwenzake, “ulitenda kosa.” Mwenzake alijibu, “sikutenda kosa.” Ugomvi ulianza na marafiki hao wawili walikasirikiana. Mmoja baadaye alisema, “Samahani naomba unisamehe.” “Na mimi naomba nisamehe pia,” alisema mwenzake. Ugomvi ulimalizika, kwa sababu ya maneno machache ya upendo.

Kuomba msamaha na kukubali kupokea msamaha ni tiba. Karl Menninger, daktari bingwa wa magonjwa ya akili kama kichaa alisema kuwa kama angeweza kuwafanya wagonjwa kwenye hospitali ya wagonjwa wa akili kuamini kuwa dhambi zao zimesamehewa, asilimia 75 ya wao wangetoka wamepona siku inayofuata. Mzee Joe alikuwa kufani kwenye kitanda cha mahuti. Kwa muda wa miaka mingi alikuwa hapatani na Bill, ambaye zamani alikuwa mmoja wa marafiki zake. Akitaka kunyosha mambo yake kabla ya kuaga dunia alimtuma Bill waongee na kumaliza mambo. Bill alipofika, Joe alimwambia kuwa anaogopa kwenda mbinguni akiwa na kinyongo naye. Kwa kusita na kwa kujikaza Joe aliomba msamaha kwa mambo aliyoyasema na kuyatenda. Alimwaakikishia Bill kuwa amemsamehe kwa makosa yote aliyomtendea. Mambo yote yalionekana kwenda vizuri mpaka hapo Bill alipojiandaa kuondoka. Alipokuwa anatoka chumbani, Joe alimuita, “Lakini kumbuka, nikipona, haya yote niliyosema hayana maana wala uzito.”

KUSALI
Mtakatifu Stefano aliinua macho juu. Alisali. Mashaka yanatazama nyuma. Wasiwasi unatazama kila upande lakini imani inatazama juu. Tunasoma katika Biblia, “Waliendelea kumpiga Stefano kwa mawe huku akiwa anasali: “Bwana Yesu ipokee roho yangu!” (Matendo 7:59). Kusali ni gharama ya kumfuata Yesu Kristu.
Sala ni jiwe linalojenga msingi wa nyumba ya ndoa. Hoja ya msingi sio kusali tu bali kusali pamoja. Mtume Paulo anawaasa, “Mnapaswa kuwa na moyo mmoja, na fikra moja.” (1 Petro 3:8). Familia ambayo haisali ni familia iliyoasi. Mwanzo wa kuteleza kwa familia ni kudharau sala hasa sala za pamoja. Kusali hakuishii katika kusali pamoja nyumbani. Wanafamilia hawanabudi kwenda kusali pamoja Kanisani pia. Katika suala la kwenda Kanisani kusali Bwana hasimwachie Bibi yake. Hasiseme, “Sali kwa niaba yangu.” Huko mbinguni hatasema, “nenda kwa niaba yangu.”  Mbinguni ni pa wote wanaume na wanawake. Hakuna anayekunywa dawa kwa niaba ya mgonjwa. Kila mtu anawajibu wa kufanyia kazi wokovu wake.

Mbinguni si pa jinsia moja tu. Sio kama mtoto Veronika alivyofikiri. Veronika mtoto wa miaka mitano alimuuliza mama yake, Jancita, “Mama, je wanaume huwa hawaendi mbunguni?” “Huwa wanaenda mbinguni.” Alijibiwa mtoto. Mama alitaka kujua kwa nini swali kama hilo linaulizwa. “Kwa nini Veronika unauliza kama wanaume wanaenda mbinguni.?” Alidadisi mama. “Ni kwa vile sijawahi kuona picha za malaika wenye ndevu.” “Wanaume huwa wananyolewa ndevu kabla ya kwenda mbinguni.” Alimjibu mama. Nguvu ya sala ya pamoja tunaiona katika maisha ya Tobia na Sara. “Tobia aliondoka kitandani, akamwambia mkewe, ‘Inuka,dada, tumwombe Bwana atuonee huruma na kutukinga salama.’ Sara akainuka. Tobia akaanza kusali: ‘Utukuzwe ee Mungu wa wazee wetu…Uwe na huruma kwake na kwangu utufikishe uzeeni pamoja!” (Tobiti 8:7) Tobia alifikia umri wa miaka mia moja ishirini na saba. Alifikia uzee pamoja na Sara.

Tuwabebe wengine katika sala. Kubeba ni kuchukua mkononi, begani au kichwani. Ni kusaidia kwa kutoa mahitaji ya lazima. Tunaweza kusema anawabeba wazazi na kuwasimamia katika mahitaji yao yote. Yesu alipokuwa amefadhaika aliomba Mungu Baba ambebe. Tuwabebe wengine katika sala tuwalete kwa Yesu
 Tuwabebe katika sala watu wa makabila mengine na mataifa mengine. Filipo na Andrea wayahudi “waliwabeba” wagiriki kuwapeleka kwa Yesu (Yohane 12: 20-21). Tuwabebe watu wa makabilia mengine tuwapeleke kwa Yesu.  Hawa Wagiriki walikuwa wanatafuta na wanaangaika. Mtanzania ambebe Mkenya katika sala. Mkenya ambebe Mtanzania katika sala. Mkikuyu ambebe Mjaluo katika sala. Mjaluo ambebe Mkikuyu katika sala. Mkikuyu ambebe Mkalenjini katika sala. Mkalenjini ambebe Mkikuyu katika sala. Tuwabebe wenzetu katika sala. Mtakatifu Monica alimbeba mtoto wake Augustini katika sala. Augustini akabadilika. Ni huyu alisema, “Jinsi nilivyo ni zawadi ya Mungu kwangu. Jinsi nitakavyokuwa ni zawadi yangu kwa Mungu.”

UNYENYEKEVU
Biblia yasema, “Akapiga magoti akalia kwa sauti kubwa” (Matendo 7:60). Kupiga magoti ni ishara ya unyenyekevu. Gharama ya kumfuata Yesu Kristu ni kunyenyekea. Kuna sababu nyingi za kunyenyekea. Kwanza sisi ni cha kupewa. “Nani amekupendelea wewe? Una kitu gani wewe ambacho hukupewa? Na ikiwa umepewa, ya nini kujivunia kana kwamba hukupewa?” 1 Kor.4:7. Mungu ametupa vipaji mbalimbali. Kuna kipaji cha lugha, kipaji cha mehesabu, kipaji cha uandishi, kipaji cha kuimba, kipaji cha kutibu na kipaji cha kucheza mpira. Lakini si busara kuwadharau wengine kwa vile unakipaji fulani. Wewe umepewa. Ya nini kujivunia kana kwamba hukupewa? Palikuwepo na Profesa aliyekuwa anavushwa na mvuvi kwenye mto. Wakiwa katikati ya mto, Profesa alimuuliza mvuvi, “Wewe mvuvi unajua kusoma?” Mvuvi alijibu, “Profesa sijui kusoma.” Profesa alisema, “Kama ni hivyo robo ya maisha yako imepotea.” Profesa aliuliza tena, “Wewe mvuvi unajua kuandika?” Mvuvi alijibu, “Profesa sijui kuandika.” Profesa alisema, “Kama ni hivyo nusu ya maisha yako imepotea.”Profesa aliuliza tena, “Wewe mvuvi unajua kuhesabu?” Mvuvi alijibu, “Profesa sijui kuhesabu.” Profesa alisema, “Kama ni hivyo umepoteza robo tatu ya maisha yako.” Wakati wanaendelea na safari upepo mkali ulianza kuvuma. Mvuvi alimuuliza Profesa, “Profesa unajua kuogelea.” Profesa alijibu, “Sijui kuogelea.” Mvuvi alisema, “Maisha yako yote yamepotea.” 

Kinyume cha unyenyekevu ni majivuno na kiburi. “Kijapo kiburi ndipo ijapo aibu.” (Mithali 11: 2)  Unyenyekevu sio kujidharau. Ni kukubali vipaji na uwezo ulio nao na kutambua kuwa hautoki kwako bali unapitia kwako unatoka kwa Mungu. USIJIVUNE SANA KINAKUDANGANYA KIOO. Dhambi ya kwanza kutendeka mbinguni ni majivuno. Lucifer aliangushwa toka mbinguni sababu ya majivuno. “Jinsi gani ulivyoporomoshwa toka mbinguni, wewe uliyekuwa nyota angavu ya alfajiri. Jinsi gani ulivyoangushwa chini, wewe uliyeyashinda mataifa!” (Isaya 14: 12) Chini ya kila kosa kuna majivuno.

Kadili tumbili anavyopanda juu ndivyo makalio yanazidi kuonekana. Kadili tunavyopanda juu hatuna budi kunyenyekea. Hawezi kusema kama mtu fulani hayupo dunia itaacha kuzunguka kwenye mhimili wake. Itazunguka. Mlima uliaibisha kichuguu mpaka vyote viwili viliponyenyekeshwa na nyota. Mwembe ukiwa na miembe unakuwa umeinama. Ni unyenyekevu. Mwembe usio na maembe hauinami. Unyenyekevu ni mama wa wokovu “...alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba. Kwa hiyo tena Mungu alimwadhimisha mno, akamkirimia Jina lile lipitalo kila jina; ili kwa jina la Yesu kila goti lipigwe...” (Wafilipi  2: 8-10).  
                                                                                                                

Monday, December 24, 2012

KRISMASI NI KRISTU KWANZA



                                    MISA YA USIKU
1. Isa 9: 2-7
2. Tit. 2: 11-14
3. Lk 2: 1-14

UTANGULIZI
Yesu anapoingia vivuli vinatoweka. Alizaliwa usiku ili kufukuza giza. Ili afukuze giza tumpe nafasi. Krismasi ni Kristu Kwanza.
MAHUBIRI YENYEWE
Krismasi ni zaidi ya mti wa Krismasi. Krismasi ni zaidi ya kadi za Krismasi. Krismasi ni zaidi ya likizo. Krismasi ni zaidi ya kubadilishana zawadi. Krismaisi ni zaidi ya kula vizuri na kunywa sana . Krismasi ni zaidi ya kuuuza na kununua. Krismasi ni zaidi ya kununua nguo mpya. Kuna mwanaume mmoja alikuwa anakoa sana Kanisani siku ya Krismasi. Tulipomaliza adhimisho la Misa nilimuuliza mke wake, “Mbona mmeo alikuwa anakoa sana Kanisani.” Nilijibiwa na huyo mama, “Yeye ni kawaida yake siku ya Krismasi akinunua suti mpya.”  Tunapokimbizana kusherehekea Krismasi tujiulize, nini chanzo cha haya yote? Krismasi ni Kristu kwanza. Krismasi ni sherehe ya kuadhimisha siku ya kuzaliwa Yesu Kristu kama wakristo wanavyoamini. “Krismasi ni Kristu, Kristu wa haki na upendo, wa uhuru na amani,” alisema Francis J. Spellman. Tukumbuke kuwa Yesu Kristo mwana wa Maria alipozaliwa alikosa nafasi katika nyumba ya wageni. Je, atabanana katika moyo wako na wageni wengine? Je atakosa nafasi katika moyo wako. Kama kwako Krismasi ni Kristu kwanza hatakosa nafasi katika moyo wako kama alivyokosa nafasi katika nyumba ya wageni.
 Tunasoma hivi katika Biblia: “Walipokuwa wakikaa huko, siku zake za kuzaa zilitimia, (Maria) akamzaa mwanawe, mzaliwa wa kwanza. Akamzungushia vitambaa, akamlaza horini, kwa maana walikosa kupata nafasi katika nyumba ya wageni” (Luka 2:7). Hakukuwa na chumba katika Nyumba ya wageni. Nyumba ya wageni ni hoteli. Inamaanisha ni sehemu yoyote ambayo msafiri aliweza kukirimiwa. Hakukuwa na chumba kwa ajili ya Yesu katika Bethlehemu ikiwa ndiyo ishara ya kukataliwa Yerusalemu. Kushughulikia likizo ya Krismasi tukamsahau Yesu ni kumyima nafasi moyoni ambao ni kama nyumba ya wageni.
 Tukiitazama Krismasi kwa miwani ya kubadilishana zawadi, “Krismasi imejikita katika kubadilishana zawadi: zawadi ya Mungu kwa binadamu-Mtoto wake; na zawadi ya binadamu kwa Mungu pale tunapojitoa kwa Mungu kwanza,” alisema Vance Havner. Krismasi ni zawadi toka kwa Mungu ambayo mtu hawezi kuifanya iwe yake binafsi bila kumshirikisha mwingine. Mshirikishe mwingine habari njema za Yesu Kristu.
 Tukitazama Krismasi kwa miwani ya mti wa Krismasi, ni zaidi ya mti wa Krismasi. “Yeye asiye na Krismasi moyoni mwake hawezi kuikuta chini ya mti,” alisema Roy L. Smith. Chini ya miti nyingi ya Krismasi tarehe 25 Desemba patakuwepo na zawadi nyingi. Katika mti wa Kalvari msalabani palikuwepo na zawadi moja lakini inazijumlisha zawadi zote- zawadi ya Mungu kwetu ya mwana wake wa pekee Yesu Kristu. Tunapochukua zawadi toka mtini wa Krismasi tukumbuke zawadi kubwa Yesu Kristu katika mti wa msalaba. Krismasi ni Kristu kwanza.
 Tukiitazama Krismasi kwa miwani ya upendo, “Kuna upendo wakati wa Krismasi kwa sababu Krismasi ilitokana na upendo. Moyo huu wa upendo na kumtukuza Mungu ubaki ukiwaka,” alisema Joseph Emms Seagram (1841 - 1919) mwingereza raia wa Canada  na mwanasiasa. Natamani moyo huu wa Krismasi tungeutia katika chupa za marashi na kutumia marashi haya kila siku. Kila siku ifanye Krismasi katika familia yako kwa kuwapulizia watu marashi ya maneno ya upendo. Namna hii Krismasi itakuwa ni Kristu Kwanza kwa vile tunaweka katika matendo upendo wake. Kuna mpiga picha siku ya Krismasi ambaye wakati anapiga picha alikuwa karibu sana na mishumaa inayowaka shati lake lilichomwa na moto. Watu walizima moto huo. Mchungaji mmoja alianzia katika tukio hilo kuhubiri. Akisema, “Kuna mmoja wetu ambaye amewaka moto kwa ajili ya Kristu.” Nasi tuwake moto kwa ajili ya Kristu si katika kuchoma nguo bali tuwake moto wa mapendo.  Yesu alikuja kuishi pamoja nasi ili baadaye tuweze kuishi naye mbinguni. Hivyo, tumtangulize tunapoadhimisha Sherehe ya Krismasi.
                                                                  
KRISMASI NI UPENDO KWA VITENDO
 “Krismasi…ni upendo kwa vitendo,” alisema Dale Evans Rogers (1912-2001) mchezaji cinema wa kike, mwimbaji na mtunzi wa nyimbo. Nakubaliana na maneno ya mtunzi huyo. Krismasi sio kisingizio cha watu kulewa, Krismasi sio kisingizio cha walinzi wanaolinda mali ya umma kutofanya kazi. Krismasi sio kisingizio cha watu kutapanya hovyo pesa na kukosa kubana matumizi. Krismasi si kisingizio cha baadhi ya wazazi kuwapokea watoto wa shule waliokuja likizo kwa shingo upande. Krismasi sio kisingizio cha kuchanganyikiwa. Krismasi ni wakati wa kufanya matendo ya upendo. Krismasi sio tu kipindi cha kufungua zawadi ni kipindi cha kuwafungia wengine zawadi. Krismasi ni upendo kwa vitendo. Krismasi ni sherehe ya kuzaliwa Bwana wetu Yesu Kristu. Alizaliwa kuokomboa ulimwengu. Ni jambo la upendo.
Kila mfuasi wa Kristu hata mwanasiasa anatakiwa siku ya Krismasi kufanya matendo ya upendo. Papa Benedict XVI Kiongozi wa juu kabisa katika Kanisa Katoliki katika kitabu chake, “Mungu ni Upendo,” aliandika, “ni lazima upendo uhuishe maisha yote ya walei, na kwa hiyo uhuishe pia kazi zao zote za siasa, ziwe pia kazi zao za ‘upendo kijamii.” Upendo pia utawale siasa. Siasa ikiwa kazi ya upendo kijamii Krismasi inakuwa ni upendo kwa vitendo. Hii ndiyo maana ya Krismasi. Mama Tereza wa Calcutta (1910-1997) mshindi wa zawadi ya Nobel 1979 alikuwa na mawazo kama haya aliposema: “Ni Krismasi kila unapomruhusu Mungu awapende wengine kupitia kwako…ndiyo, ni Krismasi kila siku unapompa tabasamu ndugu yako na kumpa mkono wa salamu.”
Juu ya kuzaliwa Yesu Kristu tunasoma hivi  katika Biblia: “Walipokuwa wakikaa huko, siku zake za kuzaa zilitimia, (Maria) akamzaa mwanawe, mzaliwa wa kwanza. Akamzungushia vitambaa, akamlaza horini, kwa maana walikosa kupata nafasi katika nyumba ya wageni” (Luka 2:7). Yesu alinyimwa nafasi katika nyumba ya wageni. Tunapokosa kutenda matendo ya upendo kwa vitendo tunamunyima  Yesu nafasi mioyoni mwetu siku ya Krismasi. “Krismasi ni kipindi cha kuwasha moto wa ukarimu ukumbini, na miale ya upendo moyoni,” Washington Irving. Bila kufanya hivyo ni kumunyima Yesu nafasi moyoni. Krismasi ni kipindi cha kuonesha ukarimu na kusamehe.
Krismasi si wakati wa watu kugombana na kutumia mabavu. Kufanya hivyo ni kumunyima Yesu Kristu nafasi mioyoni. Kuna insha iliyoandikwa na Mkurugenzi wa California Department of Mental Hygiene akionya: “Kipindi cha Krismasi kinajulikana kinasifika kwa msongo wa mawazo na matendo zaidi ya matumizi ya mabavu kuliko kipindi chochote cha mwaka.” Krismasi tofauti na ujumbe huo hakina budi kuwa kipindi cha kumwinua Yesu Kristu badala ya kuinua matumizi ya mabavu maana yeye alitetea amani. “Amani dunia itadumu, tutakapoiishi Krismasi kila siku,” alisema Helen Steiner Rice.
Hali ya hewa ya Krismasi haina budi kuwa ya upendo. Mtoto mmoja aliyepewa sanamu za kuchezea. Alilalamika kwa mama yake. Mimi naonyesha upendo kwa sanamu hizi lakini zenyewe hazionyeshi upendo. Yesu Kristu kwa kuzaliwa tuonyeshe upendo kwake. Kipimajoto cha upendo ni upendo kwa jirani zetu. Upendo kwa jirani lisiwe suala la Krismasi bali suala la maisha. Tusingoje Krismasi kupeana zawadi. Krismasi huwe utamaduni wa maisha. “Nitaiheshimu Krismasi moyoni mwangu, na kujaribu kuitunza mwaka mzima wote,” alisema Charles Dickens. Huwezi kupenda chumvi bila kupenda muuzaji wa chumvi. Huwezi kupenda Krismasi bila kumpenda Kristu. Benjamin Franklin alisema: “Watu wengi wanasheherekea siku ya Kuzaliwa Kristu! Wachache kweli, wanashika maagizo yake!” Ndugu msomaji nakutakia furaha ya Krismasi ambayo ni matumaini; roho ya Krismasi ambayo ni amani; moyo wa Krismasi ambao ni upendo kwa vitendo

Sunday, December 9, 2012

TRY THE UNTRIED WAY


Monday of the Second week of Advent
Today’s Readings
1.       Isaiah 35:1-10
2.       Luke 5:17-26
 And when they could not find by what way they might bring him in because of the multitude, they went upon the housetop, and let him down through the tiling with his couch into the midst before Jesus. And when he saw their faith, he said to him, Man, your sins are forgiven you” (Luke 5: 19-20).
When the closed door sickens you, know that there is the untried way. “When one door of happiness closes, another opens; but often we look so long at the closed door that we do not see the one which has been opened for us,” said Helen Keller-the American Author and Educator who was blind and deaf (1880-1968). In today’s Gospel we are told about the people who were carrying a paralytic man on a stretcher. The multitude blocked the door. They were unable to lay a stretcher before Jesus. And when they could not find by what way they might bring him in because of the multitude, they went upon the housetop, and let him down through the tiling with his couch into the midst before Jesus. And when he saw their faith, he said to him, Man, your sins are forgiven you” (Luke 5: 19-20). They tried the untried way. On this St. John Chrysostom had this to say, “But they are to be admired who brought in the paralytic, since on finding that they could not enter in at the door, they attempted a new and untried way.”  Do not look so long and so regretfully upon the closed door. Attempt the untried way, see the door which God has opened for you. When you bump up against a problem try the untried way. Make the adventure into the unknown. Look for the extra in the ordinary and you will find the extra-ordinary. When access is denied, try the untried. When the business is stopped, try the untried. When everything is padlocked and locked, bolted and blocked, inaccessible and impenetrable, obstructed and fastened then try the untried. There will be an opening where an opportunity is dispensed.
Prayer
 Lord Jesus Christ! You who can turn a negative into a positive, a trial into a triumph, a thorn into a rose help me to try the untried. Help me to discover an opportunity in a problem. Help me to discover a window of opportunity in a closed door. Amen.

Thursday, November 29, 2012

THE VOICE OF VICTORY



 Today’s readings:          
Rev 18:1-23, 19:1-9; Ps 100:1-5; Luke 21:20-28

With Jesus Christ, there are voices of victory, with the devil there are voices of defeat. When Jesus will come again to judge the dead and the living, there will be voices of victory. The book of Revelation tells it all:  “After this I heard what sounded like the roar of a great multitude in heaven shouting: “Hallelujah! Salvation and glory and power belong to our God, for true and just are his judgments. He has condemned the great prostitute who corrupted the earth by her adulteries. He has avenged on her the blood of his servants” (Rev 19:1-2). Don’t wait for Jesus’ second coming to hear the voice of victory. Tune in to voices of victory. What you need is selective hearing. Heaven starts from the earth, it is a continuation.
Whoever tells you that Monday is a blue Monday, that is not the voice of victory. Don’t listen to “can’t be done” voice. That is not the voice of victory. When someone is convinced that things can’t be done, he will cling to that conviction in the face of the most obvious contradiction. The story is told of the time when Robert Fulton gave the first public demonstration of his steam boat. One of those “can’t be done” fellows stood in the crowd along the shore repeating, “He can’t start it.” Suddenly, there was a belch of steam and the boat began to move. Startled, the man stared for a moment and then began to chant, “He can’t stop it.” Robert Fulton stopped it. He didn’t listen to the voice of defeat. To defeat the voice of failure, have the will to succeed. You were born to win. David Ambrose said, “If you have the will to win, you have achieved half your success; if you don’t, you have achieved half your failure.”

Counter

You are visitor since April'08