Saturday, February 4, 2017

USIJIFANYE MWANGA, KUWA MWANGA:



2017 Februari 5: Jumapili

“Ninyi ni mwanga wa ulimwengu” (Mathayo 5: 14)

 Katika hili, nyota wa zamani wa Uingereza katika runinga za Malcolm Muggeridge alisema “Siwezi sema ni kwa kiasi gani nimlipe mama Teresa. Alinionesha ukristo kwa matendo. Alinionesha upendo kwa vitendo. Alinionesha namna upendo wa mtu mmoja unavyoweza kuanzisha wimbi la upendo ambalo laweza kuenea dunia nzima”.Mama Teresa alikuwa ni mwanga wa ulimwengu ambaye aliangazaupendo kuliko kujifanya anapenda.Upendo wake haukuwa wa kujitangaza: ulikuwa ni moto wa altare.Ulitakiwa ukolezwe na upendo huo uendeleekuwaka; kwaiyo sala ilikuwa ni muhimu kwake. Mwanga unaotoka kwa Mungu, ni mali ya Mungu na unatakiwa kuangaza utukufu wake. Kamaupendo uking’aa lakini kwa mtu pekee  unaweza kuwa ni majivuno yaliyojaa kujionyesha;upendo wa Mungu ni heshima ya kweli. Katika tukio lolote tendo la utukufu wa Mungu ndiyo furaha kuu ya mwanadamu.

Martin Luther King Junior alisema, “Giza halifukuzi giza: mwanga tu unaweza kufanya hilo. Chuki haiwezi kufukuza chuki: upendo unaweza kufanya hilo.”  Upendo ni mwanga unaweza kufukuza giza la chuki. Upole ni mwanga unaweza kufukuza giza la hasira. Kuchapa kazi ni mwanga unaweza kufukuza giza la uvivu. Kuna mtu mmoja baada ya kuona anapata shida ya kusali kila wakati wa kulala kwa sababu ya urefu wa sala akaona aiandike sala yote nakuibandika ukutani, ikifika muda wa kulala anasema: Ee Mungu kama kawaida hapo ukutani,Amina! Huo ni uvivu. Wakristu walipewa sifa kubwa na Yesu alipowaita mwanga wa dunia. Lakini sifa hii inawaendea watu wote wanaotenda mema na kushinda ubaya kwa wema.
Buddha baada ya kuchunguza mshumaa alisema: “Maelfu ya mishumaa yanaweza kuwashwa na mshumaa mmoja, na umri wa mshumaa hautafupishwa. Furaha haipungui kwa kuwashirikisha wengine.” Hupotezi chochote kwa kuwasaidia wengine. “Mshumaa haupotezi chochote kwa kuwasha mishumaa mingine,” alichunguza hilo katika mishumaa James Keller. Joyce Meyer alisema hivi: “Biblia inasema kuwa Wakristo ni chumvi ya dunia na mwanga wa ulimwengu. Kazini, kwenye duka la vinywaji na hata kati ya marafiki wasio wastaarabu na wanafamilia, Watu wa Mungu wapo kuleta ladha katika hali mbaya.”
Mwanga unaonekana na unatusaidia kuona. Mfanyakazi lazima aonekane anafanya kazi. Kiongozi lazima akuone ili kupandishwa cheo. Mkristo lazima aonekane anakuwa mkristo jikoni, dukani, kiwandani, hotelini, uwanjani, sokoni, michezoni, bungeni, barabarani.

“Maneno yote yatakuwa hayafai kama hayatoki ndani – maneno ambayo hayatoi mwanga wa Kristo yanaongeza giza” (Mwenye heri Mama Teresa wa Calcutta). Kuwa mwanga wa dunia kunatudai kutumia maneno ambayo yanatoa mwanga wa Kristo.  Tunaweza kusema tusiende  mbele ya wanzetu na midomo mitupu.  Midomo ibebe maneno  yanayotia mwanga: maneno ya shukrani, maneno ya kutia moyo, maneno ya kuchangia hoja, maneno ya kusifu, maneno ya msamaha, maneno ya upendo hayo ni maneno ya kuleta mwanga. Tutafakari methali ya Poland, “Maneno yapimwe yasihesabiwe.” Yapimwe kama yanafaa au hayafai. Maneno yanayofaa yanaweza kutusafirisha kutoka kwenye matope hadi kwenye mwezi. Maneno yenye huruma ni mafupi lakini mwangwi wake unafika mbali. Matusi hayafai badala yake tumia maneno yenye huruma.
Sala: Ee Mungu naomba ulimi wangu utoe maneno yanayoleta mwanga, maisha yangu yawe mwanga wa kuwaangazia wengine, kazi zangu zikupe utukufu, watu waone wakutukuze. Amina.

Counter

You are visitor since April'08