Showing posts with label DAILY SPIRITUAL VITAMINS. Show all posts
Showing posts with label DAILY SPIRITUAL VITAMINS. Show all posts

Wednesday, May 10, 2017

KATIKA SHIDA NA RAHA, JARIBU KUSHUKURU



TAFAKARI 11/5/2017

(K)“ Watu na wakushukuru, Ee Mungu. Watu wote na wakushukuru” (Zab 67:5)

Wakati wa raha jaribu kushukuru. Zab 67 iliimbwa katika sikukuu ya shukrani baada ya mavuno (Kut23:24). Wakati wa shida jaribu kushukuru. Katika shida Ayubu alimsifu Mungu: “Bwana alitoa, na Bwana ametwaa; jina la Bwana litukuzwe” (Ayubu 1:21). Kusifu ni kushukuru. Maneno “watu wote” yanabainisha wenye raha na wenye shida, wenye nacho na wasio nacho, wagonjwa na wenye afya, walala hai na walalahoi, walalaheri na hohehahe, wanaoteseka na wanaofurahi.  Watu Wote wamshukuru Mungu. Hata unapokosewa unajifunza kitu fulani, shukuru. “Msamaha wa kweli ni pale unapoweza kusema, ‘Nashukuru kwa uzoefu huo,’” alisema Oprah Winfret. Biblia inatwaambia: “Shukuruni katika kila jambo; maana hayo ni mapenzi ya Mungu kwenu katika Kristo Yesu” (1 Wathesalonike 5: 18). Rick Warren katika kitabu chake Maisha Yanayoongozwa na Malengo alikuwa na haya ya kusema juu ya aya hiyo: “Mungu anakutaka umshukuru kwamba atatumia matatizo yako kutimiza malengo yake.”  Kutoshukuru ni kosa kubwa kuzidi kulipa kisasi. “Kutoshukuru ni kosa la kudharauliwa zaidi ya kulipa kisasi, ambacho ni kulipa baya kwa baya, wakati kutoshukuru ni kulipa baya kwa wema,” alisema William Jordan. Tujenge utamaduni wa kushukuru. Tanzania yenye utamaduni wa kushukuru inawezekana.

Mungu anapotoa hapimi kwa kijiko. Tusimbanie shukrani. Waluhya wana methali isemayo, “Nyama choma haiwezi kuwa tamu ukamsahau aliyeichoma.” Maisha yana baraka, usimsahau anayeleta baraka-Mwenyezi Mungu. Yesu alipoomba kulisha wanaume 5,000 wanaojua kula chakula Mungu Baba alimwongezea kuliko alivyokuwa ameomba wakakusanya mabaki vikapu kumi na viwili. Bikira Maria alipoomba na kusema: Hawana divai. Haikupatikana bora divai bali divai bora-grade one. Mfalme Solomoni aliomba hekima, Mungu akamwongezea na mali. Yosefu aliomba kukumbukwa. Alikumbukwa na zaidi alifanywa Waziri Mkuu. Huu ni mlipuko wa baraka. Kuna mzee fulani aliyekuwa hakosi kuhudhuria adhimisho la Misa. Jumapili moja alihamua kupanga matumizi yake. Aliweka shilingi elfu moja kwenye mfuko wa suruali kwa ajili ya kutoa sadaka na shilingi 10,000/= aliziweka kwenye mfuko wa shati kwa ajili ya matumizi madogo ya nyumbani. Wakati wa kutoa sadaka alitoa noti kwenye mfuko wa shati bila kuitazama. Baadaye alienda dukani kununua sukari na mchele. Baada ya kufunguwa bidhaa hiyo alipoingiza mkono wake kwenye mifuko alipata shilingi 1,000/=. Aimwomba samahani muuza dukani. Kwa kusononokea alienda nyumbani. Baada ya dakika tano akiwa nyumbani alikuja mtu aliyemletea pesa hili kumaliza deni lake la zamani laki tano. Mungu anapotoa hapimi kwa kilo. Kuna namna nyingi za kuwashukuru unaokaa nao.

Kushukuru ni kuomba tena. “Msijisumbue kwa neno lolote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu” (Filp 4:6).  Kushukuru ni kufanya haja zako zijulikane na Mungu. “Shukrani ni moyo wa kutegemea kupata misaada siku za baadaye” (Sir Robert Walpole). “Hakuna kazi ambayo inahitaji kufanyika haraka kama kutoa shukrani” (Mt. Ambrose). Tusishukuru kwa namna ya kuomba miujiza ya ajabu. Kuna mtoto aliyefanya mtihani wa darasa la saba. Usiku wakati wa sala za usiku alisikika akisema: “Mungu nakushukuru ulivyonisaidia kujibu maswali naomba Mwanza ugeuke kuwa Mji Mkuu wa Tanzania.” Kushukuru si kuomba kwa namna hiyo.

Kushukuru ni kuthamini. Mthamini mwenzako. Mungu wetu ni Mungu anayethamini. “Kwa kuwa ulikuwa wa thamani machoni pangu, na mwenye kuheshimiwa, nami nimekupenda” (Isaya 43:4). Wathamini watoto. Maua ya kesho yako kwenye mbegu za leo. Kuna mwalimu mmoja kila wanafunzi walipoingia darasani alisimama mlangoni akimwinamia kila mwanafunzi alipoulizwa kwa nini anafanya hivyo, alisema sijui hawa woto watakuwa wakina nani? Viongozi wangu wa kesho. Aliwathamini si jinsi walivyo tu bali watakavyokuwa. Mwanamke mmoja alimuuliza mke wake: “Mbona kila mara ninapoimba unatoa kichwa dirishani?” Mwanamke akasema: “Nataka majirani wajue kuwa anayeimba vibaya sio mimi.”

Sala: Ee Yesu nisaidie kushukuru katika shida na raha, katika magonjwa na afya, wakati wa vigelegele na wakati wa kelele. Amina.

Monday, May 8, 2017

WAKIWA NA MASHAKA NA UKRISTO WAKO, WEMA NA KAZI ZAKO VIKUSHUHUDIE


“Huko Antiokia, ndiko kwa mara ya kwanza, wafuasi waliitwa Wakristo” (Matendo 11:26)

“Kama tungetenda kama wakristo kweli, pansigekuwepo na watu ambao si wakristo,” alisema Mt. Papa Yohane XXII.  Ni katika mtazamo huo huo, Soame Jenyns alisema: “Kama nchi za kikristo zingekuwa nchi za kikristo, pasingekuwepo na vita.”  Kama ungekamatwa kwa kuwa mkristo, je pangekuwepo na ushahidi wa kutosha wa kukutia hatiani? Je, kuna ushahidi gani wa kuwa wewe ni mkristo. Mkristo kama mshumaa lazima atulie wakati huo huo anawaka mapendo. Mkristo anaonesha ukristo. Ukristo: “Ni wema nyumbani. Katika biashara ni ukweli. Katika jamii ni adabu. Kazini ni kutenda haki. Kwa wenye shida ni huruma. Ni msaada kwa wadhaifu. Upinzani dhidi ya waovu. Ni imani kwa wenye nguvu za kimaadili. Ni ‘msamaha’ kwa wakosefu. Ni furaha kwa waliofanikiwa. Ni uchaji na imani kwa Mungu,” alisema mtu fulani. Ukristo ni kuwa mkristo pale ulipo. Usipokuwa mkristo pale ulipo huwezi kuwa mkristo popote. Wanafunzi walioitwa wakristo walikuwa kwanza wakristo Antiokia.

Mtoto wa miaka minne alimuuliza mama yake: “Hivi mama Yesu unayenielezea habari zake kira mara ni mwema kama wewe? Mama alimjibu: “ Yesu ni mwema sana mimi najitahidi kumuiga.” Mtoto alijibu: “Kama ni hivyo nitampenda.” Wema ni sifa ya kuwa mkristo. Tunaambiwa juu ya mkristo Barnaba: “Barnaba alikuwa mtu mwema na mwenye kujaa Roho Mtakatifu na imani. Kundi kubwa la watu lilivutwa kwa Bwana” (Matendo 11:24).

Sifa nyingine ya mkristo ni kuwatia wengine moyo. Barnaba maana yake mwana wa kutia moyo. Alimtia moyo Paulo. Mtu akinunua pikipiki mtie moyo. Usiseme, “Inafanana na yangu.” Ukaishia hapo. Mtu akinunua nguo nzuri mpongeze. Usiseme, “Nilinunua kama hii mwaka 1970.” Mwanafunzi anayepata maksi za chini, mtie moyo. Dante Gabriel Rossetti mshairi na mchoraji maarufu wa karne ya 19 alitembelewa na mzee fulani. Mzee huyo alikuwa amebeba picha na michoro mbali mbali ambazo alitaka zihakikiwe ili kujua kama ni mizuri. Rossetti alizitazama kwa makini sana. Baada ya kuziangalia chache alisema ukweli kuwa michoro si mizuri. Mgeni huyo alisikitika sana. Alitoa michoro mingine na kumwambia kuwa imechorwa na kijana mwanafunzi. Rosseti alizitazama na kuchangamka na kuwa na furaha na kusema, “Michoro hii ni mizuri. Kijana huyo aliyezichora ana kipaji kikubwa. Apewe kila msaada na kutiwa moyo katika wito wake wa kuwa mchoraji. Kijana huyo ni nani? Ni mtoto wako?” Mzee alijibu. “Siyo mtoto wangu ila ni mimi miaka arobaini iliyopita. Kama miaka hiyo ningesikia maneno mazuri kama haya ningekuwa mchoraji mzuri sana. Hata kama watu hawakutii moyo jitie moyo. Kuna mwanafunzi ambaye alikuwa hapendwi na wenzake. Aliitwa Siima. Hata walimtania kuwa hata kivuli chake hakimpendeki hakiko tayari kumfuata. Siku moja alikuwa anaadhimisha Siku yake ya Kuzaliwa. Alijua kuwa hakuna atakayemwandikia kadi ya pongezi. Alifanya kitu fulani. Wenzake walipokuja kumtembelea na kumkejeli walikuta kadi kumi na mbili. Walishangaa. Walipozisoma zikuwa zote zinatoka kwa mtu mmoja. Kutoka kwa Siima kwenda kwa Siima.

Kazi zako zikushuhudie. “Kazi ninazofanya mimi kwa jina la Baba yangu zinanishuhudia” (Yohane 10:25). Watu walikuwa wamemuuliza Yesu kama ndiye Kristo. Kazi zake za huruma zilimshuhudia. Wewe kama ni mkristo kazi zako zikushuhudie. Matendo ya huruma yakushuhudie. Wewe kama ni daktari wa binadamu, kazi zako zikushuhudie. Wewe kama ni mwalimu kazi zako zikushuhudie. Wewe kama ni mwanasiasa kazi zako zikushuhudie. Pilato alipoambiwa kuwa kuna watu wanasema anaimba vibaya. Alijibu, “Nitafanya mazoezi na kuimba vizuri hakuna atakayewaamini.” Kazi zako zifanye watu wasiamini mabaya yanayosemwa juu yako. Kuna watu waliosema  vibaya juu ya Bwana Yesu alipokuja anakula na kunywa tofauti na Yohane Mbatizaji lakini kazi zake nzuri zilimshuhudia.

Sala: Ee Bwana Yesu nisaidie niwe mkristo kweli, niwe sauti ambayo kwayo utazungumza,niwe moyo ambao kwao utapenda, niwe mikono ambayo kwayo utasaidia. Amina.

 

JIPROGRAMU NA MWACHE MUNGU AKUPROGRAMU



TAFAKARI 8/5/2017

“Nalikuwa katika mji wa Yafa nikiomba, roho yangu ikazimia, nikaona maono” (Matendo 11: 5)

Usipojipogramu watu wabaya watakuprogramu. Mungu asipokuprogramu watu wabaya wanaweza kukuprogramu. Mungu alimprogramu Simoni Petro kupitia ndoto au maono. “Jambo hili lilitendekea mara tatu” (Matendo 10:16). Mungu anatuprogramu mara nyingi. Mungu alitaka Petro abadili mtazamo wake: Kutoka Mungu wa Israeli kwenda Mungu wa mataifa yote. Kutoka kukumbatia waliotahiriwa kwenda kwenye kukumbatia wasiotahiriwa. Kutoka kula nyama ya wanyama walio safi hadi kula nyama ya wanyama najisi kama nguruwe.  Huenda Mungu atakuletea maono kama Petro lakini unaweza kupiga picha kichwani ya mambo mazuri. Unaweza kujiprogramu.

Kuna kitendawili kisemacho: “Nimelala usiku natazama filamu.” Jibu ni ndoto. Hatuna budi kuwa na filamu ya maisha tunayoyataka akilini mwetu.  “Ni muda muafaka wa kuishi maisha ambayo umeyafikiria,” alisema Henry James. Fikiria utakapokuwa kesho. “ Tuko tulivyo na tulipo kwa sababu kwanza tulipafikiria,” Donald Curtis. Kuna mambo kadhaa ya kuzingatia.

Kuwa na picha akilini. Unataka kununua gari, kuwa na picha ya gari hilo akilini. Unataka kuoa, kuwa na picha ya arusi akilini mwako. Unataka kujenga nyumba, kuwa na picha akilini mwako ya nyumba unayoipenda.  “Roho haiwezi kufikiri bila picha,” alisema Aristotle. Tunaweza kusema mtu hawezi kufikiri bila picha. Naye John Holland alisema, “Roho haiwezi kuzungumza bila picha.” Mtu hawezi kuzungumzia mipango yake bila picha. Ukizungumzia duka unalotaka kulianzisha kuwa na picha. Ukizungumzia taasisi unayotaka kujenga kuwa na picha akilini mwako.“ Badili sura za picha kwenye kichwa chako ziendane na maono kwenye moyo wako,” alisema mtu fulani. “Piga picha ya kitu unachokitaka akilini, kione, kihisi, kiamini. Fanya picha ya kitu hicho kichwani mwako, na anza kukijenga,” alisema Robert Collier. “Kupiga picha akilini ni kuona lile ambalo halipo, ambalo halionekani – ndoto.  Kupiga picha akilini kusema kweli na kutengeneza uongo unaonekana. Uongo unaonekana, hata hivyo una namna ya kuwa ukweli wa mambo,” alisema Peter McWilliams.

Fikiri kama kwamba unachokitaka kipo.  “Kuleta jambo katika maisha yako, fikiria kama kwamba tayari lipo,” alisema Richard Bach. Yapigie msitari maneno “kama kwamba” ni maneno muhimu. “Umba maono ya unayetaka kuwa na baadaye ishi katika picha hiyo kama kwamba ni kweli,” alisema Arnold Schwarzenegger.  Ishi kama kwamba lisilowezekana linawezekana. “Watu wa kawaida huamini tu katika linalowezekana. Watu wasio wa kawaida hupiga picha si ya lile ambalo linawezekana au linayamkinika bali lile ambalo haliwezekani. Na kwa kupiga picha ya lile lisilowezekana wanaanza kuliona kama linalowezekana,” alisema Cherie Carter-Scott.

Badili unachokiona. “Toa mawazo yako, maneno yako na macho kwenye mambo yalivyo, na yaweke tu kwenye namna ambavyo unataka mambo yawe,” alisema  Che Garman.  “Mtu anaweza kupokea lile ambalo anaona anapokea,” alisema Florence Scovel Shinn. “Lazima uone kitu vizuri akilini kabla ya kukifanya,” Alex Morrison.

Kuna faida nyingi za kuwa na picha ya unachokitaka akilini.  Kwanza, picha ya unachokitaka inakupa matumaini. “Ukiwa na maono kwa ajili ya maisha yako hilo linakuwezesha kuishi kwa matumaini badala ya hofu zako,” alisema Stedman Graham. Pili, ni kupiga hatua kimaendeleo.  Hatua ya kimaendeleo inategemea upeo wako ulivyo. Upeo wako ukiwa chini hutabaki chini. Upeo wako ukiwa juu utakuwa juu kweli. “Mtu anaweza kukua kiasi ambacho upeo wake unamruhusu,” alisema John Powell. Watu wenye upeo wa juu sana si wa kawaida. Tatu, kunasaidia kufanikiwa.  Ukweli huu unabainishiwa na methali ya kichina: “Dunia ni ya wale ambao wanavuka madaraja mengi katika kufikia kwao kabla ya wengine hawajaona hata daraja moja.” Nne, kupiga picha akilini kunasisimua, na kuleta ari mpya. “Kila dakika, kila saa, piga picha kichwani namna unavyotaka uwe. Sisimukia WEWE mpya,” alisema, Thomas D Willhite. Picha akilini ni kichocheo cha kutenda. "Picha inazaa shauku. Unakusudia lile ambalo umelipigia picha ya akilini,” alisema J. G. Gallimore. “Naota kwa hiyo nakuwa hivyo,” Cheryl Grossman.

Tuesday, March 8, 2016

A HOUSE OF MERCY WITHOUT MERCY




Tuesday of the 4th Week of Lent
March 8, 2016 Reflection by Rev. Dr. Faustin Kamugisha
“Do you want to get well? “Sir,” the invalid replied, “I have no one to help me into the pool when the water is stirred?” (John 5: 6-7)

Jesus visited a famous pool. Its name was Bethesda which means House of Mercy. There was a paralytic who had been there for thirty eight years.  Desperately he tried to reach the pool but the people around the house of mercy pushed past him or brushed him aside. The man was helpless and friendless near the House of Mercy without mercy.  Jesus showed himself as the helper of the helpless and the friend of the friendless. He cured the invalid. The man’s waiting was turned into believing. He was cured. “The man might well have said with a kind of injured resentment that for thirty-eight years his bed had been carrying him and there was not much sense in telling him to carry it” (William Barclay). Nevertheless, he carried his bed.  With Jesus a house of mercy without mercy was full of mercy. Jesus is the incarnation of mercy. Let your house be a house of mercy; let your home be a home of mercy.
Prayer
 Ever Merciful God, I wish to receive mercy, help me to show mercy to my neighbours. Amen.

Monday, November 9, 2015

THE CURE FOR SELF PITY




Tuesday, 10 November 2015  

Today’s readings
1.      Wisdom 2: 23 -24; 3, 1-9
2.      Luke 17, 7-10

When you fulfill your duty there is no room for merit, self pity, pride or boasting. You have done only your duty. If you have done your duty don’t show off. “If you show off do not get upset when God doesn't show up,” said Matshona Dhliwayo, a writer from Zimbabwe. The following utterances disclose pity felt for self: what’s the use? I have sacrificed but to what purpose? Jesus in the parable of today’s Gospel rejects the idea that God owes us something. When we have done our best we have only done our duty. St. Ambrose tells us: “Boast not yourself then that you have been a good servant. You have done what you ought to have done. The sun obeys, the moon submits herself, the angels are subjects; let us not then seek praise from ourselves.”  Boast in the Lord, boast not yourself. This attitude is the cure for self pity.
Prayer,
God our Father! What I receive from you is grace and goodness, and not reward. Help me to work in quiet joy leaving the issue of reward in your hands. Amen!

Monday, October 26, 2015

DELIGHTED OR HUMILIATED




Monday of the 30th Week in Ordinary Time
October 26, 2015
Today’s readings
1.      Romans 8: 12-17
2.      Luke 13: 10-17
When something good happens, we normally find two types of groups: the delighted and the humiliated. The crippled woman straightened by Jesus was delighted. She was seen and called by Jesus, she was delighted. She, who her eyes were on the ground, after Jesus’ healing touch, she could stare silently into his eyes, she was delighted. She, who could not hold a child or be hugged after Jesus’ healing touch she could hug the child to her chest. She could give any of her relative a big hug. She was delighted. The lovers of the systems and laws more than the people were humiliated.  “The ruler preferred that this woman should like the beasts rather look upon the earth than receive her natural stature, provided that Christ was not magnified,” said St. Cyril the Father of the Church. The ruler of the synagogue was possessed of the self-made hurts. When God blesses your neighbour are you delighted or humiliated?
Prayer for Today  
Oh! Lord Jesus Christ, make me delighted at the welfare of my neighbour. Make me a brother (sister) to everyone. Amen.

Thursday, August 13, 2015

MBINGU IANZIE DUNIANI




                  SHEREHE YA KUPALIZWA BIKIRA MARIA MBINGUNI
1.  1 Mambo ya Nyakati  15: 3-4, 15-16, 16: 1-2
2. 1 Kor 15: 54-57
3. Lk 11: 27-28

Leo tunasherehekea Sherehe ya Kupalizwa Bikira Maria mbinguni. Alipalizwa hakupaa mbinguni. Ni Yesu alipaa mbinguni. Ukweli kuwa Bikira Maria alipazalizwa Mbinguni tunaupata katika Biblia kitabu cha Ufunuo, “Ishara kubwa ilionekana mbinguni, mwanamke amevikwa jua, mwezi ukiwa chini ya miguu yake, na taji ya nyota kumi na mbili juu ya kichwa chake” (Ufunuo 12:1).
 “Maria ameingia utukufu wa mbinguni, ameshirikishwa utukufu wa Mwanawe….Katika Maisha yake Maria alimfuata Mwanawe bila kumwacha hata alipokuwa msalabani. Sasa tunaona Mwana hamwachi mama yake, bali anamshirikisha utukufu wake” (MISALE YA WAUMINI, uk.871). Mwaliko leo ni kuwa mbingu ianzie duniani. Ni kama tunasema,  “Njia yote ya kwenda mbinguni ni mbinguni” (Canon Farrar). Chunga mawazo yako yanageuka kuwa maneno. Chunga maneno yako yanageuka kuwa matendo. Chunga matendo yako yanakuwa kuwa tabia. Chunga tabia yako inageuka desturi. Chunga desturi inageuka kuwa hatima yako.  “Nikichukua hatua ya kwanza nikiwa na wazo zuri, ya pili nikiwa na neno zuri, na ya tatu nikiwa na tendo zuri, niliingia mbinguni,” alisema Zoroaster.
Hata kama mbingu hauioni Mbingu ipo. Hauwezi kusema kwa vile Mungu simuoni Mungu hayupo. Kuna Profesa ambaye hakuamini kuwa Mungu yupo. Akiwa anawafundisha wanafunzi alimwambia mwanafunzi mmoja, “Ebu chungulia dirishani kama utamuona Mungu. Unaona nini?” Mwanafunzi akasema, “Naona miti nje. Naona majani. Naona watu. Naona magari.” Profesa kwa kujitapa akasema, “Nemekuambia Mungu hayupo.” Mwanafunzi mmoja akasema, “Profesa, ngoja mimi nimuhoji mwanafunzi mwenzangu.” Akaanza kumuhoji, “Unamuona Profesa?” Mwanafunzi mwenzako akasema, “Namuona.”  Anayehoji akazidi kuhoji, “Unaona mambo gani ya Profesa?” Mwanafunzi akajibu, “Naona shati, naona macho naona kichwa, naona viatu, naona mikono.” Mwanafunzi akaulizwa, “Je unaona akili yake.” Akajibu, “Sioni akili yake.” Mwanafunzi anayehoji akasema, “Hivyo profesa wetu hana akili kwa vile hauioni.” Katika mtazamo huo, hauwezi kusema kuwa hakuna mbingu kwa vile hauioni.
Papa Pius XII katika barua yake ya kipapa  Munificentissimus Deus aliandika hivi: “Mwishowe Bikira Maria asiye na doa, aliyekingwa na kila doa la dhambi ya asili, akishamaliza mwendo wa maisha yake duniani, aliinuliwa katika utukufu wa mbingu pamoja na mwili wake na pamoja na roho yake. Na alitukuzwa na Bwana kama Malkia wa ulimwengu, kwa sababu alikuwa amefanana sana na mwanawe, Bwana wa mabwana, na mshindi wa dhambi na mauti” (KKK Na. 966, LG 59).
SABABU ZA KUPALIZWA BIKIRA MARIA

1.      MUUNGANIKO NA MWANAWE
Mama na mwanawe, mwana na mama yake. “Bikira mwenye heri alitangulia katika safari yake ya imani akihifadhi kwa uaminifu muungano wake pamoja na Mwanawe mpaka msalabani, ambapo, kwa mpango wa Mungu  alisimama imara; aliteswa kikatili pamoja na Mwanawe wa pekee, na alijiunganisha kwa moyo wake wa kimama na sadaka yake. Alikubali kwa mapendo kuchinjwa kwa sadaka aliyoizaa mwenyewe. Mwishowe, alitolewa na Kristo mwenyewe akifa msalabani, kama Mama yake kwa mfuasi kwa maneno haya: “Mama, tazama Mwanao.”  (LG 58; KKK Na 964; Yoh 19: 26-27). Bikira Maria alipomchukua mimba Yesu aliunganika naye. Ilikuwa ni komunio yake ya kwanza. Akaenda kwa haraka kwenda kuunganika na Elizabeti. Unapounganika na Yesu nenda kwa haraka kuunganika na wengine.
2.      MFUASI WA KWANZA MATUNDA YA KWANZA YA UFUASI
Tunda la kwanza la kuwa mfuasi wa Yesu ni kushiriki maisha ya furaha mbinguni. Bikira Maria ni mfuasi wa kwanza wa Yesu. Hivyo alipata matunda ya kwanza ya kuwa mfuasi wa Yesu.  Katika Katekisimu ya Kanisa Katoliki tunasoma hivi: “Kupalizwa kwa Bikira Maria Mtakatifu ni kushiriki kwa namna ya pekee ufufuko wa Mwanawe, na ni utangulizi wa ufufuko wa wakristo wengine” (KKK Na 966). Tunasoma katika Injili ya Luka: “Alipokuwa anasema hayo, mwanamke miongoni mwa watu alipaza sauti, akamwambia, “Heri tumbo lililokuchukua na maziwa uliyoyanyonya.” Naye akajibu, “Wenye heri hasa wasikiao neno la Mungu na kulishika” Luka 11: 27-28). Kwa Yesu wenye heri ni wale wasikiao neno la Mungu-yaani wafuasi. Kuwa mfuasi maana yake kusikia, kuishi na kuliweka katika vitendo neno la Mungu (Mt 12: 49-50). Wafuasi wa Kristu ni wake Yesu. Wa kwanza kuwa wake Yesu ni Bikira Maria na hivyo kupalizwa akiwa wa kwanza kama tunavyosoma katika somo la pili: “Kama wote hufa katika Adamu, vile wote watapata tena uzima katika Kristo. Lakini kila mmoja kwa zamu yake; wa kwanza ni Kristo; baadaye walio wa Kristo…” (1 Kor 15: 23).
MAMBO YA KUFANYA ILI MBINGU IANZIE DUNIANI
Kwa kawaida mambo huanzia mbali. Kuna methali ya Wahaya isemayo, “Atakayekula chakula kweli unamugundua wakati wa kunawa mikono.” Namna ya kula inaazia mbali. Ndoa haianzii wakati wa kufunga ndoa. Ndoa inaanzia mbali. Kila Nyumba ni shule ya maisha ya ndoa. Mtoto wa kiume anajifunza maisha ya ndoa nyumbani. Vilevile mbingu inaanzia duniani. Maisha ya mbinguni hayanyeshi kama mvua yanaanzia mbali. Mbingu inaanzia dunia. Yesu aliyepaa kwenda mbinguni amesema, “Mimi nipo pamoja nanyi sikuzote, hata ukamilifu wa dahari.” (Mathayo 28:20).
  1. HUDUMA-TUNDA LA UPENDO NI HUDUMA
Bikira Maria alienda kwa Elizabeti kuanzisha “Kliniki” ndogo nyumbani kwa Zakaria amhudumie Elizabeti. Na namna hii Bikira Maria anakuwa mhudumu na muuguzi wa kwanza katika ustaarabu wa kikristu. Huduma yake ni changamoto kwetu. Katika kutoa huduma hauitajiki moyo wa “fulani atafanya.” “Tendo lolote la Wema ambalo naweza kumtendea mwanangu, afadhali nilitende sasa, kwa sababu sitapitia njia hii tena”, alisema Stephen Grellet. Tenda wema huende zako. Wema hauozi. Tujue kuwa: “Tunda la upendo ni huduma. Tunda la huduma ni amani” Mama Theresia wa Calcutta.
Siku ya hukumu Yesu kama Jaji anaweza kusema, Nilikuwa na njaa mlianzisha vikundi na vyama vya kusaidia waathirika mkajadili njaa yangu. Lakini hamkunipa chakula. Nilikuwa gerezani mkaenda Kanisani kuniombea na wala hamkunitembelea. Nilikuwa uchi mkajadili maadili ya kutembea uchi, hamkunipa nguo. Nilikuwa mgonjwa mkapiga magoti na kumshuru Mungu kwa kuwapa afya njema. Nilikuwa sina nyumba mahali pa kulala, mkanielezea kuna nyumba ya upendo wa Mungu lakini hamkunijengea nyumba. Nilikuwa mkiwa na mpweke mkaniacha nijiombee mimi mwenyewe. Mlionekana watakatatifu na karibu na Mwenyezi Mungu lakini bado nina njaa, niko mpweke na nina baridi sina nyumba. Ni katika msingi huu tunasema imani lazima itafsiriwe katika matendo. Imani na matendo havitenganishwi ni kama mate na ulimi.
  1. HARAKA KATIKA KUTENDA MEMA
Malaika Gabrieli alimjulisha Mama wa Yesu, Maria kuwa Elizabeti, jamaa yake, amepata mimba ingawa ni mzee na sasa ni mwezi wa sita yeye ambaye watu walimfahamu kuwa tasa (Lk.1:36). Baada ya kujua hilo, tunaambiwa Maria alifunga safari akaenda kwa haraka. Hakusitasita, hakuhairisha. Alimthamini Elizabeti. Alienda kwa haraka. Wengine husema haraka haraka haina baraka . Lakini katika mazingira kama haya: ngoja ngoja huumiza tumbo. Philimus mtu wa kusitasita alitembea siku moja kupitia kijijini. Alikutana na omba omba maskini aliyemwomba sadaka. Alitaka kumsaidia omba omba na kusema, “ndiyo, nitakusaidia baadaye.”Alipita karibu na Kanisa, alikumbuka kuwa hajasali sala zake. Alijiambia, “nitasali baadaye”. Alipoendelea na safari alikutana na bibi kikongwe ambaye alimwambia, ‘tafadhali naomba umpeleke mtoto wangu mgonjwa hospitalini. Niko peke yangu na hakuna mtu yoyote wa kunisaidia.” “Ndiyo,” Philimus alijibu, “Nitakusaidia, lakini nitakusaidia baadaye.” Baada ya kuachana na bibi huyo kikongwe alipata ajali ya kugongwa na gari na kufa papo hapo. Roho yake ikapelekwa bahari ya moto. Wakati akiungua, alimwomba Malaika, “Tafadhali nipe tone la maji.” “Ndiyo” Malaika alimwambia, “Nitakupa maji baadaye”. Halafu malaika alimwacha. Alipomwona malaika mwingine, Philimus alimsihi, “Nitoe kwenye huu moto.” “Ndiyo,” Malaika alisema kwa haraka, “Nitakutoa baadaye” Halafu  na malaika huyo alimwacha. Aliposihi malaika wengine, Philimus  alipata jibu lile lile, “Ndiyo, baadaye…” Kadiri alivyoendelea kuungua motoni alitambua kuwa Mungu husitasita kwa wale ambao husitasita. 
Kusitasita ni kuchelewesha mambo. Kuchelewa ni kupoteza muda. Kumbuka muda ni mali. Zaidi ya hayo kila dakika iendayo kwa Mungu hairudi. Tunasitasita labda kwa vile tunangojea mambo yawe mazuri. Lakini kumbuka, “Mvua ilikuwa hainyeshi Nuhu alipoanza kujenga safina,” alisema Howard Ruff.
  1. WAKIKUSIFU MSIFU MUNGU
Maria mama wa Yesu aliposifiwa na Elizabeti alimsifu Mungu. Alizabeti alisema hivi, “Umebarikiwa wewe katika wanawake, naye mzao wa tumbo lako amebarikiwa” (Luka 1:42). Maria mama wa Yesu alimsifu Mungu. “Moyo wangu wamtukuza Bwana, na roho yangu imemfurahia Mungu, Mwokozi wangu” (Luka 1:46-47). Maria mama wa Yesu hakujisifu na kujisifia. Alimsifu Mungu. Alimhimidi Mungu. Alimtukuza Mungu.  Elizabeti ni mfano wa kuigwa watu wa familia yako wakifanya vizuri, wakibarikiwa wasifu. Katika mambo yanayomuhumiza mwanamke ni mme wake kuwasifia wanawake wengine mbele yake bila kumsifia yeye na kwa mwanaume ni hivyo hivyo. Kuna mwanaume aliyemwambia mke wake, haupiki vizuri kama mama yangu. Naye mke wake alimjibu. “Na wewe hauna pesa kama baba yangu.”
Wakikusifu una kila sababu ya kumsifu Mungu kama Maria mama wa Yesu alivyofanya.  Kwanza ni Mungu wetu anayetoa. Mungu ndiye mpaji. Mungu ndiye mgawa mafungu. Maria mama wa Yesu alineemeshwa na Mungu na aliposifiwa alikuwa amembeba mwokozi mimbani. Pili tunamcha au tunamuogopa. Waogope wasiomuogopa Mungu. Tatu, kumsifu Mungu ni kuzuri na ni vema kama asemavyo mtunga Zaburi. “Msifuni BWANA; maana ni vema kumwimbia Mungu wetu, maana kwapendeza, kusifu ni kuzuri” (Zaburi 147:1).  Nne kusifu ni jambo la lazima na la kimaumbile. Mara ngapi katika uwanja wa mpira yanatoka bila breki maneno ya mshangao na ya kusifia kama lo, la-la-la-la mchezo ukichezwa vizuri. Ndivyo ilivyo katika uwanja wa dini kumsifu Mungu ni jambo la lazima la kimaumbile. Tano, tunampenda Mungu. Unaweza kusifia bila kupenda lakini hauwezi kupenda bila kusifia.
  1. JIBARIKI KWA MANENO
Maria mama wa Yesu alijisambazia baraka pia. “Vizazi vyote vitaniita mwenye heri” (Luka 1:48). Alijiambia maneno mazuri katika utenzi wake. Maneno hayo yaliumuumba anaitwa mama mwenye sifa na mama msaajabivu. Neno alibariki tu linaumba, linampa mtu sura mpya. Ni kweli alivyosema Edward Thorndike, “Rangi ufutika, hekalu huharibika, ufalme huanguka, lakini maneno ya hekima hudumu.” Maneno ya Mama wa Yesu yamedumu. Jibariki kwa maneno. Kuna msichana aliyekuwa na umri wa kuolewa msichana pekee kwa wazazi wake. Alijibariki wakati wa kusali. Alisema kuwa hatajiombea yeye mwenyewe atamuombea mama yake. Sala yake ilikuwa hii. “Ee Mwenyezi Mungu mpe mama yangu mkwe mzuri wa sura na tabia.” Kwa sala hii msichana huu alijasambazia baraka, yaani kuwa na mme mzuri wa sura na tabia. Kwa mama yake ni mkwe, kwake ni mme wake.  Panda mbegu za maneno mazuri ya kujibariki. Biblia inatoa wito huo. “Hata aliye dhaifu na aseme: ‘mimi pia ni shujaa” (Yoeli 3:10). Hata aliye masikini na aseme: Mimi ni tajiri. Hata aliye na akili za wastani aseme: Mimi nina akili nyingi sana. Hata na aliye na uzuri wa wastani aseme: Mimi ni mzuri sana. Anayejipenda atajiambia maneno hayo.
  1. UKIPATA SHUKURU
“Mungu amekupa zawadi ya sekunde 86,400 siku ya leo, je umetumia sekunde moja kusema, “Mungu Nakushukuru,” alisema William A. Ward. Ukitaka kupata miujiza shukuru kwa dogo ulilopata. “Shukuru kwa zawadi ndogo ndipo utaweza kupata zawadi kubwa.” (Thomas à Kempis).Mkumbuke Mungu. Hakuna haja ya kujidai sana sote ni “CHAKUPEWA.” “Nani amekupendelea wewe? Una kitu gani wewe ambacho hukupewa? Na ikiwa umepewa, ya nini kujivunia kana kwamba hukupewa?” (1 Wakorintho 4:7).   Kuna methali isemayo, “Aliyekupa wewe kiti ndiye aliyenipa mimi kumbi.” Na aliye na kidogo akitumie kupata kikubwa.
Soma zaburi ya 100, “Pitieni milango yake ya hekalu lake kwa shukrani, ingieni katika nyua zake kwa sifa. Mshukuruni na kulisifu jina lake.” (Zaburi 100: 4) Unapopitia mlango wa kanisa pitieni kwa shukrani. Unapopita mlango wa duka la magari pitieni kwa shukrani. Unapopita mlango wa Supermarket pitieni kwa shukrani. Unapopita mlango wa benki, pitieni kwa shukrani. Unapopita mlango wa Hospitali pitieni kwa shukrani. Unapopita mlango wa ofisi, pitieni kwa shukrani. Unapopita mlango wa duka, pitieni kwa shukrani. Unapopita mlango wa gereji, pitieni kwa shukrani.Unapoingia kwenye sehemu ya kuegesha magari, ingieni kwa shukrani. Fikiri na Shukuru. Unapopita kwenye mlango wako nyumba pitieni kwa shukrani. Unapoelekea kwenye chumba cha kulala, pitieni kwenye mlango kwa shukrani. Milionea wanaotajwa katika Biblia walikuwa ni watu wa shukrani.
  1. KUWA MMISIONARI WA UPENDO
Kama upendo wako hauwezi kupaa kwenda kuwatumikia wengine, una Mbawa ambazo zimevunjika. Upendo huanzia nyumbani. Umisionari uanzie mahali ulipo, kwenye jumuiya yako. Usikoke moto kwa mama wa kambo wakati kwa mama yako moto umezimika.
Juu ya Umisionari, Mama Theresia wa Calcutta alikuwa na haya ya kusema:
“Siku kadhaa baadaye, Maria alifunga safari akaenda kwa haraka hadi mji mmoja ulioko katika milima ya Yuda. Huko aliingia katika nyumba ya Zakaria, akamsalimu Elizabeth. (Lk.1:39-40). Mara Knistu alipoingia katika maisha yake, ona alivyofunga safari na kwenda kwa haraka kumtoa kwa wengine. Na namna gani anafanya hili. Na kwa kutenda tena kama mtumishi mnyenyekevu, akiosha, kusafisha na kupika kwa ajili ya binamu yake mzee. Masista wa Shirika letu wanaitwa Wamisionari wa Upendo (Missionaries of Charity) na kila mara ninasema kuwa Maria yeye mwenyewe alikuwa “mmisionari wa Upendo”. Mmisionari ni mtu anayetumwa kupeleka upendo wa Mungu kwa wengine; na mmisionari wa upendo anafanya hili kupitia matendo ya upendo, kama huduma za kiupendo na za kiunyenyekevu ambazo Maria alitoa kwa Elizabeth.
HITIMISHO: Mtaka cha uvunguni sharti ainame. Kuingia mbinguni hakuna njia ya mkato. Mtu mmoja wa  Ireland ambaye alikuwa amelewa na alikuwa anapenda pombe sana siku moja aliulizwa na Baba Paroko, “Mwanangu unategemea utaendaje mbinguni?” Mtu huyo alijibu, “Hilo ni jambo rahisi sana! Nitakapofika kwenye mlango wa mbingu, nitafungua mlango na kufunga. Nitafungua mlango na kufunga. Nitaendelea kufanya hivyo mpaka Mtakatifu Petro atakapokasirika na kusema, “Mike! Ingia ndani au Utoke hapo mlangoni.!’ Hivyo nitaingia mbinguni kwa urahisi. Mtaka cha uvunguni sharti ainame. Kwenda mbinguni kunahitaji kufanyiwa kazi.

Counter

You are visitor since April'08