Saturday, July 15, 2017

MAMBO YOTE HAYAHUSU UDONGO, BALI YANAMHUSU MPANDAJI PIA


2017 Julai 16 Jumapili ya 15

“Mpanzi alikweda kupanda mbegu” (mathayo 13:3)
Alexander Maclaren aliandika: “Mfano wa mpanzi, ni wa kihistoria na wa kinabii. Unaeleza uzoefu halisi wa Kristo, na unabashiri juu ya watumishi wake.” Mafanikio au kushindwa, uzuri au ubaya, mpanzi Yesu Kristo au Mungu wetu, usikate tamaa. Yesu akiwa amejaa neema  anaonesha jitihada za kusonga mbele kila mara, bila kuwa na mawazo ya kukata tamaa. Changamoto kwetu, tunapaswa kuwa kama Baba yetu wa mbinguni Mpanzi Mkuu. Lazima tuungane nae tuanze kupanda mbengu za injili zaidi na pasipo kubagua. “Unaposikia maneno, mpanzi alitoka akaenda kupanda mbegu, usifikirie kwamba ni marudio.  Mpanzi anatoka  mara nyingi kwa malengo mbalimbali; kama  kulima, kung’oa magugu, kutoa miiba au kazi nyingine yoyote, lakini mtu huyo alienda moja kwa mojakupanda. Ni jambo lilitokea kwa mbegu? Robo tatu ziliharibika, na robo moja ilibakia; lakini siyo zote kwa namna ile, lakini kwa utofauti fulani, na alivyopanda nyingine zilianguka njiani” (Mt. Yohane Krisostomu)

Shetani anatumia mbinu ifuatazo kunyakua kilichopandwa moyoni yaani neno la Mungu.  Shetani anatumia mbinu ya kutoona. Mwenye macho haambiwi tazama. Yaani mtu akiwa na haja na kitu ni juu yake kukishughulikia. Hauwezi kungoja kuletewa mambo mazuri. “Penye miti hakuna wajenzi.” Ndivyo isemavyo methali ya Kiswahili. Ni kama watu hawaoni hiyo miti. Kuna vitu ambavyo vinaweza kumfanya mtu hasione. Mazoea huleta dharau, lakini mazoea huleta upofu. Tunaambiwa, “Kutazama mtatazama, lakini hamtaona.” (Mathayo 13: 14) Chuki bila sababu au maamuzi mbele yaweza kumfanya mtu hasione mfano Nathanaeli. “Naye Nathanaeli akamwuliza Filipo, “Je, kitu chema chaweza kutoka Nazareti?” (Yohane 1: 46) Ukabila unaweza kumfanya mtu asione zuri kutoka kabila fulani. Ubaguzi wa rangi unaweza kumfanya mtu hasione jambo zuri kutoka watu wa rangi tofauti na yake, ingawa damu yao wote ni nyekundu.

Mbinu  nyingene  ya shetani ya kuondoa mbegu iliyopandwa moyoni ni kuleta shaka au mashaka. Shetani aliwaletea Adamu na Eva mashaka katika sura ya nyoka kama tunavyosoma katika Biblia.  “Basi nyoka akamwambia huyo mwanamke, “Ati! Hivi ndivyo alivyosema Mungu, msile matunda ya miti yote ya bustani?” (Mwanzo 3: 1) Shetani alimletea Yesu  mashaka, “Ikiwa ndiwe Mwana wa Mungu, amuru kwamba mawe haya yawe nikate.” (Mathayo 4: 3)  Maneno ati, eti na ikiwa ni maneno ya kuonyesha au kueleza shaka au wasiwasi juu ya jambo.  Mashaka utengeneza milima ambayo imani inaweza kuhamisha. Sala ya mtu mwenye mashaka iko hivi, “Ee Mungu – kama yupo Mungu kweli okoa roho yangu kama nina roho kweli.Amina.”

 Kuondoa hofu ni mbinu ambayo shetani hutumia kuondoa mbegu iliyopandwa moyoni. Watu hukimbia kumkwepa nyoka na nyoka hukimbia kukwepa watu.” Hiyo ni methali ya Yoruba. Inatufunulia juu ya woga na hofu. Shetani alimuondolea hofu Eva. “Nyoka akamwambia mwanamke, ‘Hakika hamtakufa.” (Mwanzo 3:4)  Shetani alipomjaribu Yesu alitaka kumwondolea hofu, “Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu jitupe chini; kwa maana imeandikwa, ‘Atakuagiza malaika zake; Na mikononi mwao watakuchukua; usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe.” (Mathayo 4: 6) Shetani alimuondolea hofu kwa kutumia Biblia. Shetani anaweza kukuondolea hofu kwa kutumia Biblia vibaya. Kuna watu wanaofanya ulevi kuwa halali kwa kutumia maneno ya Paulo kwa Timotheo, “Usinywe maji tu, bali unywe divai kidogo kwa ajili ya tumbo lako, kwani unaugua mara kwa mara.” (1 Timotheo 5: 23) Mtume Paulo wa Tarsus hapingi kunywa divai bali anapendekeza kiasi katika neno kidogo. Anapinga ulevi. Lakini kifungu hiki kinaweza kutumiwa vibaya kuendekeza tabia ya ulevi.

 Sala: Mpendwa Yesu, ulipanda Neno la Mungu kwa mapendo, uvumilivu, juhudi na bila kuchoka, nisaidie kukuiga wewe uliye mpanzi wa Neno la Mungu. Amina.

Counter

You are visitor since April'08